Sunday, 30 April 2017


Hakika kabla ya kuanza kilimo hiki nami nilikuwa na mitazamo mbali mbali hasi kuhusu uyoga; lakini kwa mafunzo na uzoefu tuliupata baada ya kuingia kwenye kilimo hiki  tuliweza kupata majibu mengi na kuondokana na mawazo hasi kuhusu uyoga na kugundua kuwa uyoga ni hazina kubwa sana ambayo umuhimu wake haujatiliwa mkazo hasa kwenye nchi zinazoendelea tofauti na wenzetu hasa nchi za Asia na Ulaya;  uyoga ni kitu cha thamani sana katika jamii na nchi zao kutokana na kujua faida za uyoga kiuchumi, kiafya na kimazingira.
Kumekuwa na mitazamo mbali mbali juu ya uyoga pori na uyoga unaolimwa; wengi hudhani uyoga unaolimwa hauna virutubisho kama ule wa porini, na je Uyoga huu hauna sumu? Je ukikosea kuulima unaweza kubadilika na kuwa sumu? Kwanini uyoga huu unalimwa na wakati tumezoea kuupata porini?, Mbegu za Uyoga zinatoka wapi?
Majibu ya mitazamo hiyo ni kama ifuatavyo.
Kuna aina nyingi za kuvu(fungi) duniani, inakadiriwa zipo aina milioni moja na nusu za fungi /kuvu, aina 64,000 tu ndio zimefanyiwa utafiti na wanasayansi duniani, na kati za hizo aina 10,000-12,000 zinaweza kutoa uyoga lakini aina 2,000 za uyoga ndizo zinazotumika kwa chakula, uyoga mwingine hutumika kama dawa za kutibu maradhi mbali mbali.
Uyoga pori na unaolimwa; mbegu za Uyoga:
Ili kuepuka baadhi ya athari za baadhi ya uyoga wenye sumu hasa ule wa porini,   wataalamu walifanya utafiti wa uyoga ili kupata uyoga usio na sumu na wenye virutubisho zaidi na unaoweza kutumia kama lishe na dawa;Ili kuepuka athari za baadhi ya uyoga sumu ambazo kwa kiasi kikubwa zinatokana na kutoutofautisha au kufananisha uyoga pori unaofanana na unaoliwa ni vizuri kulima uyoga kwa kutumia mbegu zilizofanyiwa utafiti; utafiti huu umfanywa kwa kutambua tu aina ya uyoga tu na haujafanyiwa mabadiliko yoyote ya kibailogia); na wengi hawajui kuwa uyoga pori ndio chanzo cha vijikuvu(mycelia) vinavyotumika katika utengenezaji wa mbegu za uyoga unaolimwa; na uyoga unaolimwa hauwezi kamwe kubadilika na kuwa sumu.
Dhana nzima ya kukusanya uyoga pori ni budi uendelee kwa kufuata kanuni kadhaa ambazo zimerithishwa kutoka kizazi na kizazi au kwa njia za utafiti wa kisayansi ambazo zinahakikisha kuwa uyoga unaovunwa hauna sumu. pia juhudi za utunzaji wa mazingira uendelezwe ili uyoga uendelee kupatikana kwenye mazingira yetu. na hapa nchini Tanzania wataalamu/watafiti wafanye tafiti nyingi ili tuweze kulima uyoga aina nyingi kutoka kwenye mapori yetu, kwani Tanzania tuna utajiri wa aina nyingi za uyoga ambazo zinaweza kutumika kama dawa na tiba.
Kivipi uyoga ulimwe?
Kinachofanyika ni kuwa baada ya kufanya utafiti wa mbegu pia utafiti ulifanywa juu ya mazingira ambayo uyoga pori huota kwa maana ya kwenye vichuguu,chini ya miti na kwenye miti/magogo; uyoga huota huko kwa sababu ya mazingira yana chakula/viinilishe ambao uyoga kama mmea hupata chakula chake kwani hauwezi kujitengezea chakula chake kwa njia ya usanisi wa chakula (photosynthesis) yaani kutumia umbijani (chlorophyll). Hivyo tunalima uyoga kwa kutengeneza mazingira yaleyale yanayohitajika uyoga kuoata; tunatumia masalia ya mazao kama maganda ya alizeti, karanga nk majani ya mpunga, ngano; maranda ya mbao ngumu na lakini zisizo na dawa, mabaki ya miwa,pamba nk; Tunajenga nyumba za udongo na kuuzeka na nyasi  sehemu zenye joto (sehemu za baridi haziitaji nyumba za udongo na nyasi) ili kuhifadhi unyevu nyevu na baridi kama kwenye kivuli cha miti na kwenye vichuguu, na hii ili kufanya uyoga huu uwe unalimwa kipindi chote cha mwaka tofauti na wa porini ambao unapatikana kipindi cha masika tu.
Hivyo kama nchi ingewekeza kwenye utafiti wa huu uyoga pori ungeweza kulimwa au kuyalinda mazingira na kupatikana kipindi chote cha mwaka na tungeweza kuimarisha afya na kupunguza utapiamlo nchini na hata kujenga viwanda vya dawa nk; kwa nchi za wenzetu uyoga na mazao yake ni biashara kubwa sana duniani. Na kwa taarifa tu Uyoga pori huu huu unaopatikana kuna wazungu wanakuja wanafanya utafiti wao na kuupeleka kwenye soko la dunia na kuuza kwa fedha nyingi sana.
Uyoga pori pia una nafasi katika kuongeza kipato ilimradi uvunaji wake unazingatia ubora na usimamizi thabiti ya kuwa hauna sumu na pia kuhifadhi mazingira ili uendelee kuwepo.
Kutokana na uharibifu wa mazingira, watu wengi kuhama kuja mijini na kupotea kwa utamaduni wa kula uyoga utamaduni wa kula uyoga umepotea na kutokuwa na tafiti nyingi za kuendeleza upatikanaji wa Uyoga ule wa pori kama nchi zingine; uyoga umepoteza umaarufu licha ya kuwa ni biashara kubwa duniani na ni chanzo cha lishe nzuri kutokanana virutubisho vyake Pia Uyoga  una nafasi ya kuwa chanzo cha ajira ili kukuza kipato, kukuza pato la taifa na kutunza mazingira kwa kutumia masalia ya mazao mbalimbali kuzalisha uyoga.

Herman Msagamasi
Founder&MD
HERTU Investement (HERTU Farms Project)
Cell: +255783182632
Whatsup: +255757315931
Instagram/Twitter: @hertufarms
Blog: hertufarmsblogsport.com


Related Posts:

  • OUR SERVICES Training, couching and support Through hands on experiences on or projects by observation, farm visit and lecturing help the community especially women, youth and the community groups to engage in similar Agribusiness ac… Read More
  • SEMINA YA BIASHARA, KILIMO CHA UYOGA NA UTENGENEZAJI VITAFUNWA KIBIASHARATemise Tanzania na HERTU Investment Hertu Farms kwa mara nyingine tena tunawakaribisha kwenye mafunzo yatakayowapa wajasiriamali elimu ya kuboresha biashara zao na kutambua fursa nyingi zilizopo nje ya kile wanachok… Read More
  • Health Benefits of Oyster mushrooms–Pleurotus Ostreatus Nutritional value: One cup of raw oyster mushroom provides about 28 calories and 0.35 grams of fat, 2.85 grams of protein and 2 grams of fiber. The same amount provides 361 mg of potassium, 0.095 grams of Vitamin B6 and 33… Read More
  • SIKU YA MAMA DUNIANIKatika kuadhimisha siku muhimu ya  Mama Duniani (Mother's Day) HERTU Investment/ Hertu Farms na Temise Tanzania ambao moja ya malengo yao wamejikita katika kumkomboa mwanamke hasa kiuchumi, tukiamini kuwa mwanamke kumili… Read More
  • HERTU INVESTMENT/Hertu Farms na TEMISE Tanzania tunapenda kuwatangazia wajasiliamali au vikundi vinavyopenda kuanzisha mradi wa uzalishaji Uyoga kibiashara sekta ambayo inayokuwa kwa kasi nchini baada ya kuwa na umuhimu m… Read More

0 comments:

Post a Comment

About our customers

About our customers

Popular Posts

Recent Posts

Text Widget